Thursday, November 1, 2012

MVUA ya MAGOLI Jumamosi Man United v Arsenal Old Trafford??


Alhamisi, 01 Novemba 2012 16:50
Chapisha Toleo la kuchapisha
>>ARSENAL haijashinda Old Trafford katika Mechi 8 za mwisho!!
>>RVP kuivaa Timu yake ya zamani kwa MARA ya KWANZA!!
RVP_in_RED>>PATA DONDOO na REKODI za Mechi Man United v Arsenal!
Jumamosi Novemba 3, ndani ya Uwanja wa Old Trafford, Manchester United itaikaribisha Arsenal katika moja ya Mechi za Ligi Kuu England, BPL, ambayo inangojewa kwa hamu kubwa kwani inazikutanisha Timu ambazo, kati yao, zimefunga na kufungwa jumla ya Magoli 41 katika Mechi 8 kuanzia Oktoba 20 na pia mvuto upo kumuona Nahodha wa zamani wa Arsenal, Robin van Persie, akiivaa Klabu yake ya zamani kwa mara ya kwanza tangu ahamie Man United mwanzoni mwa Msimu huu.
Bila shaka, Arsenal watakuwa na wasiwasi kumvaa Straika ambae wakiwa nae Msimu uliopita aliifungia jumla ya Magoli 37 na tangu atue Man United mtambo wake wa magoli umeendelea mtindo mmoja.
Juzi Jumanne, Arsenal walitoka nyuma kwa Bao 4-0 walipocheza kwenye Kombe la Ligi na kuifunga Reading 7-5 katika Dakika 120 za Mchezo huku Theo Walcott akipiga hetitriki.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 9]
1 Chelsea Pointi 22
2 Man United 21 [Tofauti ya Magoli 11]
3 Man City 21 [Tofauti ya Magoli 9]
4 Tottenham 17
5 Everton 16
6 Arsenal 15
7 Fulham 14
8 WBA 14
9 West Ham 14
10 Newcastle 13
MAN_UNITED-ANDO_RVP_SHINJI_EVRA+++++++++++++++++++++++WALCOTT_WILSHERE_OX
Msimu uliopita, Mwezi Agosti Mwaka jana Uwanjani Old Trafford, Arsenal walichabangwa bao 8-2 kwenye Mechi ya Ligi na Msimu huu Man United wamekuwa wakiendeleza wimbi lao la kufunga Mabao mengi kila Mechi baada ya Jumapili iliyopita kushusha kipigo cha kwanza kwenye Ligi kwa vinara wa Ligi Chelsea Uwanjani Stamford Bridge walipoifunga 3-2 lakini Siku 3 baadae, Jumatano, Chelsea walilipa kisasi kwa kuifunga Man United, iliyochezesha Kikosi cha Pili,  bao 5-4, kwenye Mechi ya Kombe la Ligi iliyochukua Dakika 120 baada ya kutoka 3-3 katika Dakika 90.
Katika Mechi 8 za mwisho kucheza Old Trafford, Arsenal hawajashinda hata moja baada ya kuchapwa na Man United katika Mechi 7 kati ya hizo na sare 1 tu.
Kimsimamo kwenye Ligi, Arsenal wapo nafasi ya 6 wakiwa na Pointi 15 na Man United wapo nafasi ya pili, Pointi moja nyuma ya vinara Chelsea, na wana Pointi 21.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
USO kwa USO-Man United v Arsenal:
-WAMECHEZA JUMLA MECHI: 214
-Arsenal: Ushindi: 78
-Man United: Ushindi 90
-Sare: 46
NYUMBANI kwa Arsenal: Mechi 101
-Arsenal: Ushindi: 57
-Man United: Ushindi 27
-Sare: 17
NYUMBANI kwa Man United: Mechi 102
-Man United: Ushindi 60
-Arsenal: 17
-Sare: 25
MATOKEO Misimu ya hivi karibuni:
2011/12:
Januari 22-Arsenal 1 Man United 2 [BPL]
Agosti 28-Man United 8 Arsenal 2 [BPL]
2010/11:
Mei 1-Arsenal 1 Man United 0 [BPL]
Machi 12-Man United 2 Arsenal 0 [FA Cup]
Desemba 13-Man United 1 Arsenal 0 [BPL]
2009/10
Januari 31-Arsenal 1 Man United 3 [BPL]
Agosti 29-Man United 2 Arsenal 1 [BPL]
2008/9:
Mei 16-Man United 0 Arsenal 0 [BPL]
Mei 5-Arsenal 1 Man United 3 [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
Aprili 29-Man United 1 Arsenal 0 [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
Novemba 8-Arsenal 2 Man United 1 [BPL]
2007/8:
Aprili 13-Man United 2 Arsenal 1 [BPL]
Februari 16-Man United 4 Arsenal 0
Novemba 3-Arsenal 2 Man United 2
REKODI-Mabao Mengi:
-2011/12: Man United 8 Arsenal 2
-1946/47: Arsenal 6 Man United 2
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

No comments:

Post a Comment