Thursday, November 1, 2012

MECHI KUPIGA VITA UMASIKINI: Ronaldo & Marafiki v Zidane & Marafiki!


Alhamisi, 01 Novemba 2012 15:50
Chapisha Toleo la kuchapisha
MATCH_AGAINST_POVERTY>>DESEMBA 19, Gremio Arena, Porto Alegre, Brazil.MATCH_AGAINST_POVERTY2
Magwiji, ambao pia ni Mabalozi maalum wa UNDP, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Ronaldo na Zidane, wamealika Marafiki zao ili kucheza Mechi maalum ya Programu ya ‘Kupiga vita Umasikini’ hapo Desemba 19 itakayochezwa Gremio Arena huko Porto Alegre, Brazil.
Katika Mechi hii ya 10 ya ‘Kupiga vita Umasikini’, Zidane na Ronaldo, ambao waliwahi kucheza pamoja Real Madrid, kila mmoja atateua Kikosi chake.
Mechi za aina zimekuwa zikichezwa kila Mwaka kuanzia Mwaka 2003, na kubarikiwa na FIFA pamoja na UEFA, huchangisha Fedha ili kusaidia vita ya kuondoa Umaskini.
Kawaida Mechi hizi huchezwa katika Miji tofauti kwa kuikutanisha Timu ya Mabalozi wa UNDP dhidi ya Timu ya Mji inapochezwa lakini safari hii huko Gremio Arena, Porto Alegre, Brazil zitakuwa ni Timu ya Ronaldo, ambae pia atashirikisha wenzake wa Brazil, dhidi ya Timu ya Zidane.
Mwaka jana 2011, Mechi kama hii ilichezwa Mjini Hamburg, Ujerumani kati ya Hamburger HSV na Timu ya UNDP ambayo walikuwemo Ronaldo na Zidane.
Wachezaji wengine waliokuwemo kwenye Mechi hiyo ni  Didier Drogba (Ivory Coast), Dida (Brazil), Serginho (Brazil), Jens Lehmann (Germany), Lucas Radebe (South Africa), Fernando Hierro (Spain), Michel Salgado (Spain), Gheorghe Popescu (Romania), Gheorghe Hagi (Romania), Luís Figo (Portugal), Fernando Couto (Portugal), Christian Karembeu (France), Steve McManaman (England), Pavel Nedved (Czech Republic), Fabio Cannavaro (Italy), na Sami Al-Jaber (Saudi Arabia).
Mapato kwenye Mechi hizi huenda katika Programu za kupiga vita Umasikini katika Nchi zaidi ya 27 za Marekani ya Kusini, Africa na Asia.
Mapato makubwa ya Mechi ya Mwaka jana ya huko Hamburg yalienda kusaidia balaa la njaa lililoikumba Kaskazini Mashariki ya Afrika, hasa Somalia.
Akiongea Zidane alitamka: “Kila tunapokutana kwa Mechi hizi tunaweza kusaidia na kuleta tofauti kwa wenye shida!”
Nae Ronaldo amesema: “Ni muhimu kuonyesha umoja ili kusaidia wale wenye janga la Umasikini!”

No comments:

Post a Comment