Wednesday, September 19, 2012

Roberto Mancini amponda Kipa wake Joe Hart!


Jumatano, 19 Septemba 2012 
Chapisha Toleo la kuchapisha
MOURINHO_NA_RONALDO_GOLI>>MAN CITY MTAFARUKU KIGONGO cha RONALDO!!
Meneja wa Manchester City Roberto Mancini amemtaka Kipa wake awache kuiponda Timu na kumwachia yeye kuwa ndie ataeihukumu Timu kufuatia kipigo chao cha jana huko Santiago Bernabeu ambapo Real Madrid walikuwa nyuma kwa bao 2-1 zikiwa zimebaki Dakika 5 na kuibuka kidedea kwa bao 3-2 huku bao la tatu likifungwa na Cristiano Ronaldo katika Dakika ya 90.
Mara baada ya Mechi hiyo ya kwanza ya Kundi D la UEFA CHAMPIONZ LIGI, Kipa wa Man City, Joe Hart, alitamka: “Huwezi kuwa bao 2-1 mbele zikiwa zimebaki Dakika 5 na kufungwa gemu. Tujilaumu wenyewe. Hatuwezi kuendelea kuzungumzia uzoefu. Tunao Wachezaji wazuri wanaochezea Timu zao za Taifa. Wanacheza gemu nyingi sana.”
Kauli hiyo ya Joe Hart imemfanya Roberto Mancini alipuke na kubatuka: “Kama kuna Mtu anaweza kuiponda Timu basi ni mimi na si Joe Hart. Joe Hart yeye abaki kuwa Kipa tu. Mie ndio Jaji na si Joe Hart!”
Kwenye Mechi ya jana, Man City waliandamwa na kubanwa sana na Real lakini walikuwa wao ndio waliotangulia kufunga kwa bao la Edin Dzeko.
Marcelo akaisawazishia Real lakini ni Man City tena waliochukua uongozi kwa bao la frikiki ya Aleksandar Kolarov katika Dakika ya 85.
Lakini mashuti ya Karim Benzema na Cristiano Ronaldo yaliwapa ushindi Real Madrid.
Mancini aliongeza: “Ni ngumu si kwa sababu tumefungwa, unaweza kufungwa na Timu kama Real Madrid, lakini zilibaki Dakika 4 na tulikuwa mbele kwa 2-1. Inashangaza. Inabidi tujiimarisha zaidi.”
Msimu uliopita Man City ilitolewa nje kwenye Mashindano haya hatua ya Makundi na Msimu huu Roberto Mancini anataka waende mbali zaidi.
Amesema: “Tumebakisha Mechi 5 kwenye Kundi na ni muhimu tuifunge Borussia Dortmund Uwanja wetu wa nyumbani. Itakuwa vigumu lakini tunataka kusonga mbele.”
=====================
RATIBA-UEFA CHAMPIONZ LIGI:
Jumatano Septemba 19
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
FC Shakhtar Donetsk v FC Nordsjælland
Chelsea FC v Juventus
LOSC Lille v FC BATE Borisov
FC Bayern München v Valencia CF
FC Barcelona v FC Spartak Moskva
Celtic FC v SL Benfica
Manchester United FC v Galatasaray A.S.
SC Braga v CFR 1907 Cluj

No comments:

Post a Comment