Friday, November 2, 2012

WENGER: “Hatumuongelei RVP, hamna kisasi! Nataka Mashabiki wamuheshimu!”


Ijumaa, 02 Novemba 2012 01:49
Chapisha Toleo la kuchapisha
>>OLD TRAFFORD Jumamosi: Man United v Arsenal!
>>MECHI ya kwanza Robin van Persie kukutana na Ze Ganaz tangu ahame!!
>>WENGER aungama: “RVP ni Denja!!”
ARSENE_WENGER-13Arsene Wenger amepoza maneno ya Mashabiki wa Arsenal kutaka kisasi kwa Robin van Persie kwa RVP_in_RED2kuihama Timu hiyo na kwenda Manchester United wakati Timu hizo zitakapokutana Jumamosi Uwanjani Old Trafford kwenye Mechi ya Ligi Kuu England na hiyo ikiwa mara ya kwanza kwa Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal kukutana na Timu yake ya zamani tangu ahame.
Wenger amewataka Mashabiki wa Arsenal watakaokuwepo Old Trafford kumwonyeshea heshima Robin van Persie na si kumkashifu na kumtukana.
Wenger alitamka: “Kwetu, muhimu ni matokeo na uchezaji wetu. Hatumzunguzii kabisa Van Persie. Natumaini Mashabiki watamuheshimu kwani kachezea kwetu Miaka minane na alifanya vizuri sana!”
Alihoji: “Tunapiga vita Ubaguzi, Wiki iliyopita ilikuwa hivyo na kwa nini isiwe sasa?”
Akiichezea Arsenal, Robin van Persie, mwenye Miaka 29, aliifungia Arsenal jumla ya Mabao 132, 37 yakiwa Msimu uliopita na kuwawezesha kushika nafasi ya 3 kwenye Ligi.
Wenger amesema: “Daima unataka uongoze Watu vizuri wawe na maisha mazuri! Wakifanikiwa unaridhika, sidhani kwake nilifanya vibaya!”
Hadi sasa, kwa Kipindi kifupi, Van Persie ameifungia Man United Bao 7 kwenye Ligi na yeye na Demba Ba wa Newcastle ndio wanaongoza kwenye Ufungaji.
Hilo halikumshangaza Wenger ambae ametamka: “Sishangazwi na yeye kufanya vizuri. Man United ina Wachezaji wazuri sana, na Robin ni mjanja kwenye boksi, mwenye kasi na kujua nafasi huashangaza! Wapo Wachezaji wazuri na Robin atanufaika tu. Robin ni Straika hatari sana!”

No comments:

Post a Comment