Wednesday, September 19, 2012

JANA Arsenal oyee, City chini, LEO Man United, Chelsea kipi?


Jumatano, 19 Septemba 2012 17:50
Chapisha Toleo la kuchapisha
FERGIE_na_SIMUKwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI leo Timu mbili za England, Mabingwa watetezi Chelsea na Manchester United, wataingia dimbani, wote wakiwa nyumbani, kuanza Mechi zao za Makundi baada ya jana wenzao, Manchester City kucheza na kufungwa 3-2 na Real Madrid, na Arsenal kuifunga Montpellier ya Ufaransa bao 2-1.
=====================
RATIBA-UEFA CHAMPIONZ LIGI:
Jumatano Septemba 19
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
FC Shakhtar Donetsk v FC Nordsjælland
Chelsea FC v Juventus
LOSC Lille v FC BATE Borisov
FC Bayern München v Valencia CF
FC Barcelona v FC Spartak Moskva
Celtic FC v SL Benfica
Manchester United FC v Galatasaray A.S.
SC Braga v CFR 1907 Cluj
=====================
Leo, Chelsea, wakiwa Stamford Bridge, wataanza utetezi wa Taji lao kwa kucheza na Mabingwa wa Italy Juventus ambayo kawaida huwa haishindi Nchini Uingereza kwani katika Mechi zao 11 za mwisho kucheza huko wamefungwa 8 na kutoka sare 3.CHELSEA_ULAYA_2012A
Lakini Juventus ya sasa inao Wachezaji wazoefu kama vile Kipa Gianluigi Buffon, Giorgio Chiellini na mchawi Andrea Pirlo.
Katika Mechi yao ya mwisho ya Ligi, Serie A, Juve waliipiga Genoa bao 3-1 kwa bao za Emanuele Giaccherini, Mirko Vucinic na Kwadwo Asamoah.
MAN_UNITED-ANDO_RVP_SHINJI_EVRANao Manchester United katika Mechi yao ya nyumbani Old Trafford na Galatasaray ya Uturuki watakuwa wakiweka rekodi ya kucheza kwa Miaka 18 mfululizo kwenye michuano hii ya Klabu Barani Ulaya.
Pia, upo uwezekano wa Straika wao mahiri, Wayne Rooney, akacheza sehemu ya Mechi hii baada ya kuanza tena mazoezi Siku kadhaa zilizopita baada ya kupona jeraha la kuchanwa pajani.
Mastaa wengine wanaotegemewa kuichezea Man United kwa mara ya kwanza kwenye michuano hii ni Wachezaji wapya Robin van Persie na Shinji Kagawa.
Pia, majeruhi wa muda mrefu, Kiungo Darren Fletcher, nae yupo kwenye Kikosi.
Galatasaray wao watawakosa Wachezaji wao wazoefu Mabeki Tomas Ujfalusi na Sabri Sarioglu lakini inao Wachezaji kadh

No comments:

Post a Comment